Tuesday, January 22, 2013

WALIMU WAFUNDWA KUTUMIA UFUNDISHAJI WA MUHAMO WA RUHAZA- KIGOM

Na Magreth Magosso,Kigoma

Walimu wa shule za msingi wanaofundisha katika Manispaa ya Kigoma Ujiji,wanapigwa msasa wa siku saba ili kubaini  stadi za matumizi ya muundo mpya wa ufundishaji wa muhamo wa ruhaza ambao utasaidia kudhibiti tatizo la wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika.

Hayo yamebainishwa juzi na Ofisa Elimu shule za msingi Manispaa ya Kigoma Ujiji ,Shomari Bane ambapo
 imeanza kuendesha semina ya mafunzo hayo, kwa walimu kutoka shule mbalimbali za manispaa hiyo ili   kukabiliana na tatizo la wanafunzi wanaomaliza darasa la saba wasiojua  kusoma na kuandika.
 
Hata hivyo kwa upande wake  Naibu Mkaguzi wa elimu katika manispaa ya Kigoma Ujiji, George Ngwila alisema kuwa zipo sababu mbalimbali ambazo zinachangia katika kuwafanya wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kufaulu mitihani yao ya mwisho  kutokana na ushirikiano duni baina ya  walimu, wazazi na wanafunzi wenyewe.
 
Ngwila amedai siku saba za kupewa elimu hiyo itasaidia walimu hao marejeo ya nini wanachopaswa kufanya katika utendaji wao darasani  hasa suala la kuangalia muundo wa kusoma, kuandika na kuhesabu ili  kuondoa tatizo hilo.
 Mwalim Domiciana Peter  ambaye amefundisha shule mbalimbali za msingi katika manispaa hiyo kwa miaka mingi alidai kuwa, kubadilishwa kwa mitaala kumechangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya wanafunzi wamalize elimu ya msingi wakiwa hawajui kusoma na kuandika.
 
Amesema kuwa kwa mfumo wa sasa wa mitaala  haina stadi zile za KKK na ufanyaji wa mitihani wa kuchagua unawapa nafasi baadhi ya wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kuweza kupenya na hatimaye kuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari.
 
Ikumbukwe kuwa,zaidi ya wanafunzi47 waliomaliza shule ya msingi katika shule za manispaa hiyo 2012 walikuwa hawajui kusoma,kuandika wala kuhesabu,ingawa jitihada zimeanza walimu kupewa njia yakinifu ili kukabiliana na changamoto hiyo,lidara ya elimu ipeleke walimu wao mafunzoni kila wabadilishapo mitaala.
 

No comments:

Post a Comment