Monday, January 21, 2013

KAFULILA: MASHINE ZA UCHIMBAJI VISIMA ZITAPUNGUZA ADHA YA MAJ



              Na Magreth Magosso : Kigoma
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini David Kafulila amewataka wananchi wa jimbo lake,watarajie ujio wa mitambo na mashine ya kuchimba visima ifikapo April Mwaka huu ili kupunguza adha ya maji iliyokuwa ikiwakabili kwa miongo 13.
 
Akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma ya Wanawake wa kijiji cha Kabuyange kata ya Ilagala Jimbo la Kigoma kusini kumshutumu Mbunge huyo kwa kuwatelekeza na adha ya maji ambayo inawakabili kununua maji hayo, ambapo dumu la lita 20 huuzwa kwa sh.150 zaidi ya miaka 13.
Kafulila aamekiri jimbo lake linakumbwa na kadhia hiyo,ingawa alidai adha ya maji ni katika wilaya sita za mkoa wa kigoma ,ambapo zinazopata huduma hiyo ni 27% tu,huku akibainisha mkakati wa kufanikisha kupunguza adha hiyo April 2013,pindi mitambo na mashine zitakapowasili kutoka kwa wadau wake Nchini China .
 
"kweli wananchi wanateseka hasa kinamama ambao huathirika na zoezi la utafutaji wa maji kwa umbali mrefu huku baadhi ya watoto wa kike wakipata mimba kwa kusubiri foleni ya maji, ya kisima kimoja tu kijijini hapo,nawananchi waliowengi hushindwa kumudu ununuzi wa maji,kutokana na hali ngumu ya kimaisha" alisema Kafulila.
 
Aidha alidai kuwa,ili kumaliza tatizo la maji katika mkoa wa kigoma ni pamoja na kutumia mto malagarasi kwa kutandaza mtandao wa maji,ambao utasaidia kwa asilimia miamoja kigoma kuondokana na kadhia hiyo.
 
Akizungumzia kadhia hiyo Madina Abeid (mwananchi) amesema,wamekuwa wakiitwa kwenye vikao vya kijiji ili kuelezea changamoto zinazowakabili katika kijiji hicho,ikiwemo kero ya maji   na walishachangishwa sh.3,000 lakini haipatiwi ufumbuzi wa aina yeyote na wakijaribu kumhoji mtendaji wa kijiji fedha zilipo adai amepeleka ila hajui hatma yake..
 
"mimi sielewi kabisa hii shida ya maji itaisha lini hapa kabuyange,kisima kipo kimoja kiangazi hii maji ya foleni ,hivyo tunanunua maji ya m to malagalasi serikali nayo kupitia halmashauri wako kimya shida yetu" alisema kwa huzuni Abeid.
 
Hamisa Nungu aliongeza kwa kubainisha kuwa,wananchi walifarijika kumpata kiongozi kijana ambaye atasaidia wazazi wake waondokane na kadhia hiyo ya miaka kenda,lakini huzuni ya kusaka maji kila kukicha katika kijiji cha ilagala imebaki kuwa sugu.
 
Kutokana na mkakati wa Mbunge huyo,wananchi wa kata hiyo wasubiri mkao wa kunufaika na ujio wa mitambo na mashine za uchimbaji wa visima kulingana na maeneo yenye uwepo wa maji ikiwa ni sehemu ya kupunguza kadhia hiyo.
   

No comments:

Post a Comment