Tuesday, July 16, 2013

WAISLAM WAASWA KULIOMBEA TAIFA KATIKA KIPINDI HIKI CHA RAMADHAN

Waumini wa dini ya Kislamu wakiswali
Waislamu nchini wametakiwa kutumia kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhan kuliombea Taifa liepukane na majanga na migogoro mbalimbali, ikiwamo ya kidini na kisiasa liwe la amani na utulivu.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Hajji Kavan, Muhammad Jaffa Pirali, alisema hayo alipongumza na waandishi wa habari katika mashindano ya usomaji wa Qur’an, yaliyofanyika katika viwanja vya Mwembe Yanga, jijini Dr es Salaam.

Alisema Tanzania ni nchi ya amani na utulivu hivyo kuna haja ya kuiombea iendelee.

“Waislamu wengi tunaamini huu ni mwezi wenye neema na baraka kubwa, hivyo tunaweza hata kuutumia kwa kufanya maombi ya kudumisha amani na utulivu nchini kwetu ingawa maombi yanaweza kufanyika siku zote hata kama siyo mwezi wa Ramadhani” alisema Pirali.

Alisema katika siku za karibuni kumetokea migogoro na matukio mbalimbali nchini hali iliyosababisha kuonekana Tanzania haina amani, lakini kwa kudra za Mwenyezi Mungu matatizo hayo yanaweza yasijitokeze tena.

Aliwataka wanaofanya vitendo vya uchochezi kwa maslahi yao binafsi kwa kuwafanya Waislamu kuingia katika migogoro ya kidini na madhehebu mengine kuachana na tabia hiyo kwa kuwa vinapelekea madhara makubwa kwa Taifa.

“Waislamu tunapenda amani na hakuna sehemu yoyote katika Qur’an inavyowataka Waislamu kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani, hivyo tuipukane na wachochezi wanaotaka kutuingiza katika migogoro

No comments:

Post a Comment