Monday, January 21, 2013

Mikakati ya kuweka amani mashariki mwa Kongo

Mikakati ya kuweka amani mashariki mwa KongoWakuu wa majeshi wa nchi wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu ya Afrika na Jumuiya ya Ustawi ya Kusini mwa Afrika SADC wamekutana mjini Kampala Uganda na kuweka mikakati ya kijeshi yenye shabaha ya kuwatokomeza wanamgambo  waasi walioko katika eneo  lililogubikwa na machafuko la mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Maafisa hao wa kijeshi wamesisitiza juu ya kufanya juhudi za kuleta amani na uthabiti katika eneo hilo baada ya kuonekana dalili za kushindwa juhudi za kimataifa za kuutatua mgogoro huo. Crispus Walter Kiyonga Waziri wa Ulinzi wa Uganda amesema kwenye kikao hicho kwamba kuna ulazima wa kukurubishwa mitazamo kwa lengo la kutatua migogoro iliyoko katika eneo hilo. Wakuu wa nchi za eneo la Maziwa Makuu ya Afrika wanavituhumu vikosi vya Umoja wa Mataifa vya kulinda amani nchini Kongo kwa kushindwa kuchukua hatua za kimsingi za kuzuia wimbi kubwa la mamia ya maelfu ya wakimbizi wa Kongo linaloelekea katika nchi za Uganda na Rwanda.  

No comments:

Post a Comment