Monday, January 28, 2013

UCHAWI WACHANGIA KUENDELEZA UBADHILIFU WA MAPATO TRL KIGOMA


Na Magreth Magosso,Kigoma

Shirika la Reli Tanzania Kituo cha Kigoma,imeshindwa kudhibiti mtandao wa kuhujumu mapato yake kwa kuogopa mtandao wa uchawi.
Kauli hiyo imejitokeza Kigoma ambapo Naibu waziri wa uchukuzi Mh,Charles Tizeba alipolitembelea shirika hilo kukagua utaratibu wa uongozi huo kwenye usafirishaji wa abiria na mizigo ambao ulikuwa na mapungufu mbalimbali ikiwemo viongozi kutumiwa na mtandao huo wa uchawi ambao huwaroga baadhi ya viongozi wao .
Fanuel Rugonzibwa ambaye ni Mkuu wa Kituo hicho alisema ,mtandao huo unachangiwa na viongozi walioko juu kuwapa jeuri ya kufanya jambo lolote bila kufuata sheria na taratibu za kazi kuwategemea waganga wao,kwa watakaokiuka matakwa yao.
Alidai,kutokana na hali tete ya kukithiri mtandao huo ambao hudiriki hata kuvujisha siri ya vikao vya utawala na kwa viongozi ambao wanamsimamo wa kutetea haki na stahiki za abiria ambao wanateseka na kudhulumiwa haki za msingi ikiwemo kuuziwa tiketi juu zaidi ya kiwango cha serikali cha sh.19.100.
Akichangia katika hilo Askari Polisi wa Reli mkoani hapa Koplo.Michael amedadavua kuwa,mtandao huo unaongozwa na vijana wawili Said Ngururka na Majaliwa Zuberi wamekuwa wakifanya hujuma hizo za kuuza tiketi zaidi ya bei husika na kuvujisha siri za kituo hicho na kutoa taarifa za uongo kwa uongozi wa juu ambapo huwachukulia sheria wafanyakazi wake bila kufanya uchunguzi wa kina.
Akijibu tuhuma hizo Mh,Dkt Tizeba amemtaka mkuu wa kitengo cha polisi cha reli kuwa,atakapopata taarifa ya wababe hao kuzengea maeneo ya kituo hicho siku za kusafirisha abiria watiwe nguvuni ili wachukuliwe hatua za kisheria na kufikishwa mahakaman sanjari na sheria kuchukua mkondo wake, ili iwe fundisho kwa wale wote wanahujumu shirika hilo.
" mtandao wa kichawi utafanyiwa kazi,pia wafanyakazi wa reli muone uchungu na shirika hili,acheni udokozi wa fedha za abiria wasio na tiketi na kugawana fedha za mizigo ambayo haikubainishwa katika kitabu cha risiti "alisema Tizeba.
Naye mkuu wa wilaya Kigoma Ramadhani Maneno amewashauri watendaji wa shirika hilo wajitume kwa dhati ili kuwaunga mkono waziri wa uchukuzi Mh,Harrison Mwakyembe na Naibu wake Dkt.Tizeba ikiwa na tija ya kuwarudishia imani wananchi wake ,kwa kuwaondolea adha ya urasimu wa upataji wa tiketi na gharama za usumbufu wa ughahirishaji wa safari hasa waishio mbali na manispaa ya Kigoma Ujiji. 

2 comments:

  1. UPUUZI UPUUZI UPUUZI UPUUZI UPUUZI UPUUZI HAKUNA POINT HAPA

    ReplyDelete
  2. HUWEZI KUMJUA MCHAWI KAMA WEWE MWENYEWE SI MCHAWI. UCHAWI HAUWEZI KUMSHIKA MTU MPAKA NAYE AWE AMEJIHAMI, HUYO ANAYEAMINI UCHAWI NAYE UJUE KAJIHAMI SANA NDO MAANA ANAWAJUA WACHAWI. HABARI HII HAIFAI HATA KUCHAPISHWA NA MUUNGWANA.

    ReplyDelete