Tuesday, March 5, 2013

ZAIDI YA WATU 20 WAPOTEZA MAISHA NCHINI KENYA KATIKA MASHAMBULIZI MUDA MFUPI KABLA YA UCHAGUZI



WAKATI Ushindani mkali ukiendelea kati ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya ukizidi kuwa mkali zaidi kati ya Waziri Mkuu wa nchini hiyo Raila Odinga na Uhuru Kenyatta watu zaidi ya 20 wakiwamo askari polisi tisa waliripotiwa kuuwawa  baada ya kuvamiwa na kikundi cha watu zaidi ya 200 huko Mombasa na Kilifi saa chache kabla ya Wakenya kuanza kupiga kura jana.
Saa chache kabla ya uchaguzi huo, askari polisi tisa waliuawa katika mashambulizi yaliyotokea kwenye miji ya Mombasa, Kilifi na Kwale na kuacha wavamizi wapatao 10 na raia wa kawaida watatu pia wakifariki.
Baada ya vifo hivyo, serikali ilipeleka vikosi vya askari kutoka Mariakani Barracks kwenda kutuliza ghasia hizo wakati kundi lingine la askari lilitoka Nyali Barracks ili kuweka doria katika miji ya Mombasa na North Coast.
Taarifa zilizopatikana baadaye jana zilisema kuwa kwenye mji wa Mombasa askari polisi wanne waliuawa na watu zaidi ya 100 waliovamia kituo cha kura cha Miritini.
Polisi pia ilithibitisha kuuawa kwa watu saba katika mapigano hayo huku na wengine kadhaa kutiwa nguvuni.
Wavamizi wengine waliuawa katika miji ya Kisauni na Kilifi huku polisi wanne wakiuawa Chumani na mmoja huko Chonyi huku watu watatu wakiuawa kwa kupigwa risasi.

No comments:

Post a Comment