Wednesday, March 27, 2013

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUDUMISHA AMANI NCHINI



Na Shaffiru Makosa & Muharami Matenga- kigoma

Wakati jitihada mbalimabli zikiendelea kufanywa na serikali kwa lengo la kudumisha amani  na upendo miongoni mwa wanajamii ya watanzania Kaimu  sheikh mkuu wa mkoa wa Kigoma wa baraza kuu la waislamu Tanzania bakwata Alhaji Hassan Kibulwa  ameunga mkono hatua hiyo ya  kudumisha amani na upendo nchini kwakuwataka viongozi wa dini kutekeleza maazimio mbalimbali ya vikao vya  mabaraza ya mahusiano mema vinanavyo shirikisha viongozi wa dini zote kwa lengo la  kudumisha  amani na upendo ha pa nchini.

Alhaji kibulwa ameyasema hayo katika kikao maalum cha baraza kuu la waislamu Tanzania bakwata mkoa wa kigoma kilichoshirikisha viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali kwa shabaha ya kujadili mustakbali wa amani ya mkoa huu  ikiwa ni pamoja na kutafuta ufumbuzi wa  migogoro ya kidini  inayoendelea kushika kasi  katika baadhi ya maeneo hapa mkoani Kigoma .insert ….

Alhaji Kibulwa amekemea tabia ya baadhi  viongozi wa dini wa kiislamu wanaotumia maandamano kama silaha ya  kuishinikiza serikali kutekeleza madai yao jambo ambalo ni kwenda kinyume  kabisa na mafundisho ya mtume muhamadi (s.a.w)

Licha ya shekhe kibulwa kuwataka viongozi hao wa  dini ya kiislamu  na wakiristu kutataua changamoto  zinazohatarisha mahusiano ya waumini wao  kwa njia ya kidiplomasia   pia akatoa wito kwa viongozi hao kujishughulisha katika kutafuta ufumbuzi wa chanagamoto za kimaendeleo kwa waamini wao ikiwemo za  kielimu  na kiuchumi badala ya kujikita katika masuala ya kiimani pekee.

Kufuatia hatua hiyo ya kaimu Sheikh wa Mkoa wa Kigoma  ya  kuunga mkono zoezi la kudumisha amani nchini baadhi ya viongozi  hao wa dini  katika  mkutano huo wakatilia mkazo juhudi hiyo kwakulitaka baraza la waisalamu Tanzania bakwata kukaza buti katika kushughulikia harakati za kimaendeleo nchini ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha waumini wake bila kujali mipasuko ya kimadhehebu.

No comments:

Post a Comment