Monday, March 18, 2013

MGOGORO WA KAFULILA NA MBATIA WAKOMA: KAFULILA AREJEASHWA KUNDINI BAADA YA KUOMBA RADHID

David Kafulila
Na Magreth Magosso, Kigoma

Mbunge wa jimbo la Kigoma kusini, David Kafulila wa chama cha NCCR-Mageuzi ameomba radhi kwa chama chake, baada ya kugundua makosa yake yaliyopelekea kutaka  kuvuliwa ubunge na hatimaye kwenye chama hicho.

 Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Taifa  wa chama NCCR-Mageuzi Samweli Ruhuza wakati akihutubia  maelfu  ya wakazi wa kata ya  Nguruka kwenye mkutano wa hadhara wa kuhamasisha wananchi wajiunge na chama hicho,ambao  ulifanyika  viwanja vya shule ya msingi Nguruka   na kubainisha  utovu wa nidhamu alioufanya mbunge huyo na mkakati wa kumaliza tofauti hizo ili kukiimarisha chama.

"ule mgogoro  baina ya  Mwenyekiti Mhe.Mbatia na mbunge wenu  hivi sasa haupo, na wanafanya kazi kwa kushirikia  ili kujenga chama chetu kiweze kuwa imara na chenye nidhamu" amesema  Ruhuza huku wanachama wapya 153 wakichukua kadi kujiunga chama hicho.

Ruhuza alidai kuwa Mhe.Kafulila ametafakari na kugundua kuwa alichokuwa anakifanya si sahihi na ili kumaliza nongwa akamua kuomba radhi sanjari na  masharti  ikiwa na tija ya kutimiza vigezo fulani  ambao kwa hivi sasa ameshakamilisha kwa mujibu wa katiba na taratibu za chama.

Aidha halmashauri kuu ya chama hicho kilikaa katika kikao chake mwezi wa tisa mwaka jana na kupokea ombi la msamaha wa Mhe Kafulila na kukubali ombi hilo la kumsamehe,huku halmashauri kuu itakaa tena kikao mwezi wa nne tarehe sita ili kuweka bayana uhalali wa kurudishwa kundini kwa mbunge huyo.



Amedai kuwa, lengo la uongozi wa chama kutaka kumfukuza uanachama Mhe.Kafulila halikuwa la kiutashi wa maslai binafsi la! bali ni kutaka kujenga nidhamu ndani ya chama  ambayo ndio msingi  wa awali   kwa miaka kenda hivyo hakuna mwanachama anayeweza kuwa juu ya sheria ya katiba ya  chama hata siku moja na ikifika hatua hiyo ni kheri ajifuke mwenyewe.


No comments:

Post a Comment