Thursday, February 28, 2013

DROGBA RUKSA KUKIPIGA KLABU BINGWA ULAYA


Benedikt Howedes and Didier Drogba
DIDIER Drogba ruksa kuitumikia Galatasary ya Uturuki kwenye michuano ya kombe mabingwa Ulaya baada UEFA kutupilia mbali malalamiko ya Schalke ya Ujerumani.
Nyota huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 34 alicheza mechi yake ya kwanza ya Ulaya dhidi ya Schalke Februari 20 katika mzunguko wa kwanza ulioishia kwa matokeo ya 1-1.
Schalke walilalamika kuwa mhezaji huyo hakusajiliwa katika muda muafaka kumuwezesha kucheza michuano ya Ulaya iliyofikia hatua ya mtoano.
Hata hivyo UEFA imetupilia mbali malalamiko hayo ambayo kama yangetia hatiani Galatasaray basi ingekwenda katika mechi ya marudiano ikiwa nyuma kwa bao 3-0 kwa mujibu wa kanuni za UEFA.

No comments:

Post a Comment