Wednesday, April 17, 2013

UGUMU WA MASOMO, NA UKOSEFU WA FEDHA NI BAADHI YA SABABU ZA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU KUJINYONGA


Ubakaji, Ushirikina na matatizo ya kifamilia navyo vyachangia kujinyonga

“ Nafikiri ni wakati muhimu kuanzisha madarasa  maalum ya saikolojia,  ili kuwaweka sawa wanavyuo.  Nasema hivyo kwa sababu uamuzi wa kujiua ni sehemu  ya maradhi ya akili,’’anaeleza
Waandishi  Peltzer Karl na Paswana Nancy katika  kitabu chao, Suicidal behaviour among South African university students: Contributing factors, resources and prevention,  (Sababu na namna ya kuzuia vifo vya kujiua kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vya Afrika Kusini), wanataja sababu zinazochangia matukio ya kujiua kwa wanafunzi hususan wa  vyuo vikuu vya Afrika Kusini, ikiwamo ugumu wa masomo na masuala ya kijamii.

Sababu nyingine ni ukosefu wa fedha, matatizo ya kifamilia, imani za kishirikina, kubakwa, kuwa waathirika wa virusi vya Ukimwi, kufiwa na ndugu na jamaa, na tabia binafsi.
Aidha, kwa mujibu wa  Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Afya (WHO), zaidi ya asilimia 90 ya vifo vya kujiua duniani vinatokana na matatizo ya akili kama vile kuwa na msongo wa mawazo,  unywaji pombe uliopitiliza na skizofrenia (magonjwa ya akili)

Ufumbuzi wa tatizo

 Taarifa nyingi zinaonyesha wanafunzi wa vyuo vikuu katika maeneo mbalimbali ni moja ya makundi mwathirika wa matukio ya kujiua. Bila shaka elimu, hamasa na misaada mbalimbali inatakiwa kutolewa vyuoni ili kulinda kundi hili muhimu katika jamii. 
Huduma za ushauri  hasa masuala ya kisaikolojia vyuoni hazina budi kuanzishwa,  kuimairishwa na kuwa rafiki ili kuvutia idadi kubwa ya wanafunzi wanaokabiliwa na matatizo husika.

No comments:

Post a Comment