Saturday, December 15, 2012

UKATILI WA KIJINSIA KWA WANAWAKE HAUKUBALIKI

Mkuu wa idara ya mawasiliano ya umma (SAUT) Bi Imane Duwe (picha kubwa katikati)  akiwa ktk kongamano la  jinsia na afya ya uzazi lililoandaliwa na wanafunzi wa mawasiliano ya umma mwaka wa tatu SAUT lililofanyika katika ukumbi wa Mgulunde chuoni hapo.
moja ya sababu zinazowafanya wanawake wa kati ya umri wa miaka 17-25 watoe mimba kwa kuhofia kupoteza shepu ya maumbile yao. pia wamekuwa wakitoa mimba kuwa sababu ya kuwa na wapenzi wasio wa kudumu.
Tanzania inachukua nafasi ya tano duniani kwa wanawake kufanya kazi mbalimbali bila kupata malipo (ujira) kwa kazi mbalimbali wanazozifanya. Hayo yamesemwa na Bi Khadija Liganga (kulia) toka kivulini wakati akiwasilisha mada ktk kongamano la jinsia na afya ya uzazi lililoandaliwa na wanafunzi wa shahada ya mawasiliano ya umma mwaka wa tatu ktk chuo cha SAUT.

No comments:

Post a Comment