Saturday, December 8, 2012

MLIPUKO WA BOM WAJERUHI WATU 10 NCHINI KENYA


http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/6595d83c54ff005f9781fab0904b75ac_XL.jpg


Polisi ya Kenya imetangaza kuwa, watu wasiopungua 10 wamejeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea karibu na Msikiti mmoja huko Nairobi mji mkuu wa nchi hiyo. Baadhi ya duru nyingine za habari zinaeleza kuwa, watu watatu wameuawa kwenye mripuko huo. Polisi ya Kenya imeeleza kuwa, mripuko huo umetokea katika eneo la Eastleigh, eneo ambalo wakazi wake wengi ni Wakenya wenye asili ya Kisomali. Siku ya Jumatano iliyopita, mtu mmoja aliuawa na wengine wanane kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko wa bomu pambizoni mwa barabara katika eneo hilohilo la Eastleigh. Hadi sasa hakuna mtu au kikundi chochote kilichotangaza kuhusika na milipuko hiyo.

CHANZO: Idhaa ya kiswahili ya tehran

No comments:

Post a Comment