Tuesday, April 9, 2013

UHURU KENYATTA AAPISHWA RASMI KUWA RAIS WA NNE KENYA.


  • Rais Kikwete amtaka Uhusu Kenyatta aingie Ikulu kama Rais na si kama mtoto aliyekulia Ikulu ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa sababu kukulia Ikulu ni tofauti na kuishi kama Rais wa nchi.


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiejWThb2LRRGsTpS-30c9zNierakfYGadQQfBbkqg2U3aGm20qtvT1eMJIgMtwdWMo1BevfHn5CwCmY9uPDqHp2QWNNi0KR9zVbz_mo7Px4CE37EERo7K7f63xKzqoF-oEfJkBrWZ8NENn/s1600/164287_10151195580187609_1571565168_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEivra0vJZQOpl2EBoRqDpzTlIn8_hHeyVL39lcKAW36yN1gzdnrN7fNm2-CcagdYga15iC8VUUSHr66x-xKrgs7XhnSTOUhZ-RpvbtO7-JQCpGW4rKFYwbFCWClcd8ltMZb7PcAyqk9pd3d/s1600/64844_10151195579017609_1383596097_n.jpgRais Uhuru Kenyatta akila kiapo cha Urais,kuwa rais wa awamu ya nne nchini Kenya,kwenye sherehe zilizofana kwa kiasi kikubwa ndani ya uwanja wa kasalani.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgHdUTXmhjcprqo1M-Fn9kuzyIeWyFnKTx0jFprvACI_3pFgQ3z6keldMdeOC4N8rs7ZVkivawuErV4gMLRSIGMS60EEy1E-BibVGb7cWBfnWum0amtu6pwH4dZknhpIb4dEjfi4qluUl7d/s1600/547497_10151195583982609_1581134814_n.jpgRais mpya wa awamu ya nne nchini Kenya,Mh Uhuru Kenyatta akiwapungia maelfu ya watu waliofika kushuhudia kuapishwa kwake, mapema leo kwenye sherehe iliyofanyika kwenye uwanja wa Kasarani,jijini Nairobi Sherehe hizo zimehudhuriwa na Marais kutoka nchi mbalimbali akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh Jakaya Mrisho Kikwete,Mabalozi mbalimbali na watu mbalimbali.Picha zote kwa hisani ya Mike Kariuki wa Capital FM.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidXlo_5Lr4Z3blVAsy5Rt8ahqfIET6FcOPYi56m91eEsYUnZRGywZ0USXDWpaxyLFn42zFTLHth6pTUBKY4c_JnU_OVYAEWN8yRiE_dLNB1nJeku3ZsH7khQZqkZFUCx49XrRLFCsFQngM/s1600/529085_10151195578917609_1205076097_n.jpg
Rais Uhuru Kenyatta akisalimiana na Makamu wake William Ruto.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgo-iBCuJDeVAGyTUymEahZpaf_jTe-K1E_la4P1jk5Zb6EiihWUZJxIKBFuFM1j5pb932ggmgnrU-pFZZTrzwA_yVbem6Z_A_l7BQ4Yd6q-4kIF6bzBo3Ul9TxBzAc6SFZFD5rAerkNP4W/s1600/11691_10151195578622609_363234948_n.jpg
Rais wa Uganda,Mh Yoweri Kaguta Museven akisoma hotuba yake fupi wakati wa kuapishwa kwa Rais wa awamu ya nne nchini Kenya,kwenye sherehe zilizofanyika ndani ya uwanja wa Kasalani,jijini Nairobi.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjWqL11shWRzEsfKalP06zZfbX1javNuFWVURsiXhPtc-gtIekUPathyicpUNSgiFW-s1765DmB1R15rUu56fuT3EkXRqnKTNKm4gyYTwJ_rI7RWvEtL3GNM_CFhycY6Jwga0f8Y696uJlc/s1600/524443_10151195579592609_804760154_n.jpg

Akizungumza baada ya kuapishwa kuwa rais wa nchi hiyo alisema kwamba suala la amani ya nchi hiyo ndiyo itakuwa ajenda ya kwanza katika utawala wake.
"Ndugu zangu wakenya, suala la amani ni suala muhimu sana, kulinda amani ya nchi ni ngumu kuliko kuzua vurugu mdani ya nchi,napenda kuwahakikishia kwamba amani itaendelea kutawala Kenya na kamwe sitapenda kuona mtu yoyote akijaribu kuivuruga amani yatu"alisema Rais Kenyatta.
Kuhusu suala la ajira nchini humo alisema,"Kazi ya pili itakayofuata ni kazi ya kuhakikisha kwamba watu wasiokuwa na ajira wanapata ajira ndani ya nchi kwani kwa kipindi kirefu wakenya wamekuwa wakikosa kazi huku wataalam mbalimbali wakitoka nje ya Kenya" , Kwa upande wake Makamu wa Rais William Ruto alisema kwamba huu ni muda wa kuwatumikia wakenya na hiyo ndiyo kazi iliyopo mbele yao.
Naye Rais wa Tanzania  Jakaya Kikwete akitoa salamu kwa niaba ya viongozi mbalimbali walioalikwa katika sherehe hizo alimtaka Kenyatta aingie Ikulu kama Rais na si kama mtoto aliyekulia Ikulu ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa sababu kukulia Ikulu ni tofauti na kuishi kama Rais wa nchi, huku pia akimwakikishia ushirikiano mkubwa katika jumuia ya Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment