Wednesday, April 3, 2013

VURUGU ZA KIDINI ZAIBUKA TUNDUMA, MSIKITI WACHOMWA MOTO


Mapigano makubwa yameibuka hii leo baina waislam na wakristo katika mji wa Tunduma Wilayani Mbozi Mkoani Mbeya na kusababisha msikiti mmoja kuchomwa moto katika maeneo ya Mwaka na Kisiman

Vurugu hiyo iloyodumu takriban masa manne imeilazimu Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha kutuliza Ghasia (FFU) kuingia mitaani na kupiga mabomu ya machozi kila mahali huku akitoa amri yakuwataka wananchi kuingia ndani na kulala mchana huu.
Chanzo cha virugu hizo inadaiwa kuwa imetokana na mzozo wa uchinjaji nyama ambao Rais Kikwete aliutole ufafanu na kusema kwamba burasa itumike katika kutatua mzozo huo.

Akizungumza  mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alisema kwamba mbali na mabomu ya machozi kupigwa ovyo, barabara zimefung, maduka yamefungwa huku matairi yakicchomwa moto barabarani.

No comments:

Post a Comment