Monday, February 11, 2013

PAPA BENEDICT XVI ATANGAZA KUJIUZULU NAFASI YAKE February 28 MWAKA HUU


Akitangaza maamuzi hayo Papa Benedict alisema ameamua kujiuzuru kwa sababu hana nguvu tena za kuendelea na majuku yake ya ofisi.
Papa Benedict mwenye umri wa miaka (85) alisema kwamba amekuwa na maamuzi hayo ya kujiuzuri tangu mwezi uliopita.
"Nimefikia kiwango ambacho siwezi tena kuendelea na majukumu yangu ya kutoa huduma na siwezi kutimiza majukumu yangu ipasavyo ofisini” alisema kupitia taarifa yake iliyotolea na Msemaji wa Vatican.

Papa Benedict anatarajia kukabidhi ofisi  yake rasmi february 28 mwaka huu.
Papa Benedict amekuwa wa kwanza kujiuzuri nafasi hiyo tangu Kanisa la Roma duniani kuweka utaratibu wa kuongozwa na kiongozi huyo kwani Papa hutakiwa kulitumikia Kanisa hilo mpaka atakapofariki dunia.

Hatua hiyo itatoa mwanya kwa Kanisa katoliki kufanya uteuzi wa Papa mwingine atakayechukuwa nafasi yake
CHANZO:  Reuters

No comments:

Post a Comment