Sunday, February 10, 2013

UTALII WA NGONO WASHAMIRI NCHINI


Vijana wa kitanzania wawapagawisha wanawake wa kizungu, na kuwa vivutio vya utalii huo
 “apewe mpaka apagawe, atoe tiketi.” ni kaulimbiu inayotolewa na vijana hao kupata tiketi ya kwenda ulaya.
 Kumeibuka aina mpya ya utalii, unaojulikana kama utalii wa ngono, ambao unashamiri kwa kasi ukihusisha zaidi watalii wanawake wanaofuata wanaume wa Kitanzania hasa vijana.
Uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwa utalii huo unaongezeka kwa kasi hasa katika maeneo yenye vivutio vingi vya utalii ikiwamo Arusha, Kilimanjaro na Zanzibar.
Wanawake hasa watu wazima walio na umri kati ya miaka 60 hadi 80 kutoka nchi mbalimbali, wamekuwa wakiingia nchini kwa lengo la kutafuta vijana wa kiume wa kustarehe nao.
Uchunguzi huo unaonyesha kuwa wanawake ambao hawana vigezo vya uzuri vinavyopendwa na wanaume huko kwao, ikiwamo wembamba na urefu, husafiri kuja Tanzania kutafuta mwanamume atakayestarehe naye kingono.
Hali hiyo inawakumba zaidi wanawake wanene, ambao kwa Ulaya hukosa wapenzi, hivyo kulazimika kusafiri kuja Afrika Tanzania ikiwamo kutafuta mwenza wa kustarehe nao.
 Utalii huu umeshamiri nchini, ambapo vijana wa Kitanzania wanaufahamu na kukiri kuwa umewanufaisha na baadhi yao kuwasaidia kupata tiketi za kwenda kuishi Ulaya.
Katika Visiwa vya Zanzibar utalii huo unafanyika zaidi katika fukwe za Nungwi, Kiwengwa, Paje, Kendwa, Jambiani na maeneo mengine yaliyopo pembezoni mwa bahari.
Katika fukwe hizo vijana maalumu kwa kazi hiyo, wana kauli mbiu yao inayosema:“apewe mpaka apagawe, atoe tiketi.”
Kwa kauli mbiu hiyo vijana hao wanamaanisha kuwa, kwa kila mwanamke watakayekutana naye, watatumia kila mbinu ili kumfurahisha hadi awasafirishe au kwenda naye Ulaya.
Abdulla Ali Haji (Sio jina halisi) ni miongoni wa vijana wanaojihusisha na aina hiyo ya utalii, akiishi visiwani humo ambapo anaeleza kuwa shughuli yake kubwa ni kuzunguka katika fukwe mbalimbali akiwinda wanawake wa kizungu wanaotaka kustarehe.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment