Friday, February 22, 2013

FINANCIAL TSUNAMI -TIJA KWA AFRIKA WABADILISHE MFUMO WA KIBENKI


 

Na Magreth Magosso,Kigoma
IMEBAINIKA kuwa, Mfumo wa kuwekeza fedha Benki  kwa  Riba ni anguko la viwanda vya kimataifa na kudumaa kwa uchumi wa Nchi za Afrika.
Kauli hiyo imebainishwa  na Mkurugenzi  wa  huduma ya benki isiyo na riba NBC  Yassir  Masoud  Kigoma Ujiji  jana  kwenye warsha ya wadau wa uwekezaji wa fedha katika mabenki mbalimbali  wakibainishiwa  mfumo wa riba na athari zake na chukizo kwa mungu  ikiwa na tija ya kufuata  mfumo usiokuwa na riba ( Islamic Banking) ambao  unaridhiwa na mungu  kwa wananchi wa imani zote za dini hali itakayochochea  kupanda kwa uchumi wa  mmoja mmoja sanjari na  kukua kwa huduma za  wananchi .
“Mfumo wa kuwekeza bila riba unaepusha ugomvi baina ya benki husika na mteja ,wateja wengi wanauziwa thamani zao kutokana na kushindwa kulipa riba ya fedha alikyokopeshwa,sasa itumieni huduma hii ambayo hata mataifa ya magharibi ikiwemo marekani ,malasia,Singapore wamebaini hili wanatumia  mfumo kama Islamic banking msitishike na jina ni kwa wote wahitaji” alibainisha Masoud.
Meneja  wa  NBC-Tawi la Kigoma  Mathias  Mhangilwa alisema kuwa,mfumo wa Islamic Banking ni uwekezaji wa fedha unaolenga uhalisia wa maumbile ya mwanadamu ambao unauadilifu kwa mafundisho ya vitabu vyote vinakataza riba haimanishi ni kwa ajili ya imani ya kislamu tu ni kwa kila mdau  huku akiwataka  wafanyabiashara wa kigoma wachangamkie fursa hiyo ili waboreshe tija zao.
“ World Bank inafanya mchakato wa kuhakikisha kuna sera  ya mfumo huu usiokuwa na riba ,pia mfumo huu hauna anguko la kiuchumi kwani anguko ni chachu ya fedha haramu ya riba watanzania tumechelewa  kujiunga na mfumo huu,lakini sasa utumieni ili nchi yetu isiyumbe kiuchumi ikiwa mataifa ya magharibi yataanguka cha ajabu 30% waliwekeza mfumo huu ni wakristo na 2% waislamu msihofu ” alisisitiza Mhangilwa.
Khadija Katumba  na Asha Issa walidai kuwa,kutokana na elimu waliyoipata  toka kwa NBC-Isalamic Banking ,juu ya adha ya  mikopo ya riba watakuwa mabalozi wa elimu hiyo kwa wanawake wathubutu wa kufanya biashara waachane na mfumo wa udhalilishaji ambao wengi wameuziwa majumba yao kutokana na riba ambaye ni sawa na mdudu wa kansa kwa kumaliza uchumi wa wajasiliamali wasio na elimu juu ya mikopo ya riba.
Ikumbukwe kuwa,wadau wa uwekezaji ni wahanga wa kufilisiwa thamani zao na Benki mbalimbali za hapa nchini pindi wanaposhindwa kulipa deni la mikopo, hali iliyopelekea Benki ya Taifa NBC kuanzisha huduma hiyo ambayo kwa sasa unatumiwa ulimwenguni na mataifa ya magharibi na Asia wakijaribu kufutu (Financial Tsunami) anguko la kiuchumi siku za usoni kwa mujibu wa mwanazuoni wa zamadamu  bara la Asia anayejulikana kama Ibn Qayyim Jawziyya.

No comments:

Post a Comment