Monday, July 8, 2013

WATU 53 WAMEUAWA KATIKA MASHAMBULIZI YA KIJESHI NCHINI MISRY


Haya yanajiri huku ghasia zikiendelea baada ya kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa rais Mohammed Morsi
Chama cha Brotherhood kimwarifu kuwa watu 53 wameuawa na wengine zaidi ya 500 wamejeruhiwa kwa kupigwa risasi mjini Cairo nje ya kambi ya jeshi la nchi hiyo.


Habari zinadai kuwa watu hao ni wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi waliokua wamekusanyika nje ya kambi hiyo ya jeshi wakipinga kuondolewa madarakani kwa rais Morsi.

Wizara ya Afya ya Misri imetaja idadi ya waliouawa kwenye mashambulizi hayo ya jeshi ya leo kuwa watu 40. Watu walioshuhudia wameeleza kuwa jeshi la Misri limetumia silaha hai kuwatawanya wafuasi wa Muhammad Morsi huko katika mji wa Nasr mashariki mwa Cairo. 

Kundi la Muslima Brotherhood limewataka raia wa Misri kuwapinga wale linawaita wanaopokonya raia uhuru na demokrasia. 
Brotherhood imelaumu jeshi kwa kuwaua raia wake.
Katika kikao na waandishi wa habari, wafuasi hao walimlaani vikali mkuu wa jeshi Abdel Fattah Al-Sisi na kumtaja kama muuaji aliyewashambulia raia wenzake.
Waandamanaji hao wanasema vikosi maalum viliwafyatua risasi baada ya swala ya fajir huku wengine wakishambuliwa walipokusanyika nje ya makao ambako bwana Morsi anadhaniwa kuzuiliwa wakitaka watawala kumwachilia huru.

Chama cha Brotherhood  kinasema kuwa  wafuasi wake wameuawa wakati jeshi la Misri lilipoushambulia umati wa watu hao waliokuwa wameketi chini nje ya kambi zao wakipinga kitendo cha kupinduliwa Rais Muhammad Morsi.

No comments:

Post a Comment