Saturday, December 21, 2013

KIKWETE AWAFUTA KAZI MAWAZIRI MZIGO, NI BAADA YA KUSHINDWA KUSIMAMIA WIZARA ZAO IPASAVYO

  •  Walishindwa kusimamia Operesheni Tokomeza Ujangili
  • Wananchi 13 na Askari 6 waliuawa katika opesheni hiyo
  • Ubakaji, Unyanyasaji na uporaji vilitawala katika Operesheni hiyo

Na. Butije Hamisi

Rais Jakaya kikwete hatimae amekubali ushauri wa wabunge na kuwavua nyadhifa za uwaziri mawaziri watatu na kukubali kujiulu kwa waziri wa maliasili na utalii baadaya kutuhumiwa kushindwa kusimamia Operesheni ya Tokomeza Ujangili iliyokuwa imejaa unyana na  ukatili dhidi ya raia wasio na hatia.

Akitangaza uamuzi huo wa rais ambe yuko nchini Marekani kwa matibabu wariri mkuu Mh. Mizengo Pinda alisema rais Kikwete ametengua uteuzi wa mawaziri wanne ambao ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamisi Kagasheki, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa  Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David Mathayo.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Ripoti ya Kamati ya Maliasili, Ardhi na Mazingira iliyowasilishwa jana asubuhi bungeni mjini Dodoma, kuonesha kuwa mawaziri hao waalishindwa kusimamia ipasavyo OTU ambayo ilijawa na vitendo vya ukatili, unyama, na dhulma dhidi ya wananchi wasiokuwa na hatia.

Kabla ya Pinda kutangaza hatua hiyo iliyochukuliwa na rais aliyekuwa waziri wa maliasili na utalii Khamisi Kagasheki alitangaza kujivua wadhifa huo sa 2:09 usiku alipokuwa akichangia majumuisho ya ripoti ya kamati hiyo iliyowasilishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo James Lembeli ambaye ni Mbunge wa Kahama (CCM).
“Mimi ni mtu mzima nimesikia hisia nzito sana kwa waliyoyasema wabunge.  Rais Kikwete aliponiteua ilikuwa ni kwa furaha yake na operesheni hii, yaliyotokea yametokea hali ya wanyama huko si nzuri ... nachukua fursa hii kuteremka ngazi hii ya uwaziri na nitachukua taratibu za kawaida kuijulisha sehemu inayohusika(Rais).” alisema Kagasheki.
Operesheni hiyo inadaiwa kukabiliwa na vitendo vya ukatili, unyanyasaji na mauaji ya wananchi na wanyama.
Akiwasilisha ripoti ya Kamati ya Maliasili, Ardhi na Mazingira Mwenye kiti wa kamati hiyo James Lembeli aliituhumu wizara ya maiasili na utalii kuwa imekithiri rushwa kiasi kwamba inakuwa vigumu kupmbana na kutokomeza ujangili nchini hivyo kutaka watendaji wakuu wa wizara hiyo kuchukuliwa hatua stahiki

 “...Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii nao wawajibishwe kutokana na kuhusika kwao na unyama uliotokea kwenye mpango wa Operesheni Tokomeza Ujangili. Rushwa iliyopo ndani ya wizara hiyo ni kubwa inakusanywa kwa kutumia simu, hivyo Serikali izichunguze simu zao kuanzia leo.” Alisema Lembeli.
Wakichangia ripoti hiyo wabunge waliitaka serikali kuwawajibisha mawaziri ambao waira zao zilihusika katika operesheni hiyo kuhu wengine wakienda mbali zaidi na kumtaka waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda ajiwajibishe kisiasa na wengine wakitaka kama mawaziri hawakuwajibika basi bunge livunjwe ili ufanyike uchaguzi mwingine.
MICHANGO YA WABUNGE
Mbunge wa Longido, Lekule Laizer (CCM), alitaka Bunge livunjwe endapo Waziri Mkuu na mawaziri hao watatu(Kagasheki, Nchimbi na Nahodha) watakataa kujiuzulu kwa lengo la kung’ang’ania madaraka.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), alisema hakuna jinsi ya kuonyesha namna wabunge walivyokasirishwa na vitendo hivyo zaidi ya Serikali nzima kwa maana ya Pinda kujiuzulu.
“Naomba Waziri Mkuu uchukue ‘political responsibility’ (uwajibikaji wa kisiasa) na siyo kwamba kwa kufanya hivyo anahusika la hasha… Kama hachukui hatua Bunge libebe dhamana hiyo,” alisema Zitto.
Akichangia bungeni Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia alibainisha kutuhumiwa kwa wabunge  kwenye ripoti hiyo kwa kujihusisha na ujangili na kuhujumu operesheni hiyo.
“Bungeni kazi yetu, sisi Wabunge ni kuisimamia Serikali kwa hiyo wale wabunge waliotajwa kwenye ripoti watajwe ili nao wawajibike ili Bunge letu liwe na nia thabiti ya kuisimamia Serikali,” alisema Mbatia.
Ripoti hiyo ilibainisha Operesheni ya Tokomeza Ujangili ilisababisha mauaji ya watu 13 na askari sita, utesaji wa kutisha wa watuhumiwa, ubakaji, rushwa na uporaji wa mali za wananchi.
..............................
Maoni:- 0752231172
Email: b2jhms@gmail.com

No comments:

Post a Comment