Tuesday, May 21, 2013

CHANGUDOA: WABUNGE NDIO WATEJA WETU, WANAFUNZI WA VYUO NA RAIA WA NJE WAVAMIA BIASHARA YAO


WAKATI Serikali ikitafuta kila njia ya kukomesha biashara ya ngono, hali imezidi kuwa tete jijini Dodoma baada ya kundi la makahaba kutoka ndani na nje ya nchi kupiga kambi katika mitaa mbalimbali ya jiji hilo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti mjini Dodoma wafanyabiashara hao walidai kwamba biashara yao imevamiwa na wanafunzi wa vyuo vikuu pamoja wengine kutoka nchi jirani za Kenya na Uganda.

"Wanafunzi wamevamia wateja wetu, ambayo wengi wao ni wabunge, na tumekuwa na wakati mgumu kwa sababu wanafunzi hao wanamvuto zaidi kutoka na umri wao kuwa mdogo,maumbile mazuri zaidi yetu, ingawa gharama zao ni kubwa kuliko gharama zetu, lakini bado wanatuzidi ujanja"alisema mama wa makamo anayesomesha watoto wake kwa kutumia biashara hiyo.

Mama huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mariam (35) alidai kwamba awali alikuwa akifanya biashara hiyo jijini Dar es Salaam na kituo chake kikuu ilikuwa ni Kinondoni Makaburini na alilazimika kuhamia mjini Dodoma miaka miwili iliyopita na kupata mafanikio makubwa kupitia biashara hiyo.

Uchunguzi wa kina uliofanywa umebaini maeneo ambayo yana wasichana wengi ambao ni makahaba ni Chako Nichako, Double H na Mtaa wa Uhindini ambako kuna nyumba maarufu kwa kufanya biashara hiyo haramu ya ngono.

Kahaba mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Anastazia (20) ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) alisema kwamba viwango vyake ni kati ya   sh 200,000 kwa tendo moja bila kulala sh 300,000  kwa mchepuo mmoja wakati wa kulala na akitaka michepuo miwili na zaidi ni tsh 400,000 hadi 500,000 wakati wale wamama wakubwa wanajiuza kwa tsh 30,000 hadi 50,000 tendo moja.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Nchimbi alishatangaza kuwawinda na kuwatia kwenye mikono ya sheria wale wanaojihusisha na biashara hiyo haramu. Hata hivyo, kauli hiyo inaonekana kukosa mashiko kwani biashara hiyo inazidi kushamiri siku hadi siku.

CHANZO: http://habarimpya.com

No comments:

Post a Comment