Tuesday, August 20, 2013

NEWS OF RWANDA: RAISI KIIKWETE SI MTANZANIA, ASILI YAKE NI BURUNDI



Kufuatia sinto fahamu iliyopo kati ya Rais wa Tanzania Dr. Jakaya Kikwete na Rais wa Rwanda  Paul Kagame mtandao wa kinyarwanda uitwao News of Rwanda umetoa taarifa inayomtuhumu Raisi kikwete kuwa si mtanzania bali ni raia wa burundi.
Katika tuhuma hizo mtandao huo umeshindwa kuonyesha ushahidi wa kiukoo na familia kuthibitisha tuhuma hizo baili ulijikita zaidi kwa kuangali historia kuwa Bagamoyo (Nyumbani kwao na Raisi Kikwete) ilikuwa ni kitovu cha biashara ya utumwa A. Mashariki hivyo baadhi ya watumwa kutoka Rwanda na Burundi walibakia Bagamoyo na kuanzisha makazi na hatimae familia.
Pia mtandao huo umeandika kuwa mke wa Raisi Kikwete Mama Salma Kikwete ni ndugu wa aliyekuwa raisi wa Rwanda Juvenal Habyarimana aliyeuawa kwa ajali ya ndege iliyotunguliwa mwaka 1994 nchini Rwanda. Kwa taarifa zaidi bofya hapa chini. 
bofya hapa

No comments:

Post a Comment