Friday, September 27, 2013

TUVITUNZE VYANZO VYA MAJI

Tweetter conv.

WARIOBA: "HAKIKISHENI KATIBA MPYA NI YA MAONI YA WANANCHI" ASEMA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA INAMAPUNGUFU

 
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko, Jaji Joseph Warioba amesema Watanzania hawatatendewa haki kama itapatikana Katiba Mpya ambayo haijatokana na maoni yao. “Hakikisheni Katiba Mpya inayopatikana ni ya maoni ya wananchi,” alisema jana muda mfupi baada ya kumaliza mkutano wake na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana
.
Jaji Warioba alisema maoni yaliyomo katika Rasimu ya Katiba yametokana na maoni ya wananchi, hivyo lazima yalindwe ili kudumisha amani... “Kilichomo katika Rasimu ya Katiba ni maoni ya wananchi, wasije wakafanya makosa ya kutoa maoni haya. Haya yametoka kwa wananchi na wao ndiyo watakuwa na sauti ya mwisho kuhusu mchakato huu,” alisema na kuongeza: “Wahakikishe kwamba mawazo yaliyotolewa na wananchi yanaingia katika Katiba Mpya, wasithubutu kuyatoa maana wananchi wanaweza kukataa hali hiyo.”

 Wakati wananchi wa kada mbalimbali wakishinikiza Rais Jakaya Kikwete kutokusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba 2013, kwa maelezo kuwa una kasoro, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba naye amesema sheria ina upungufu.