Thursday, November 28, 2013

MADUDU YA MTIHANI WA MOKO YASABABISHA WANAFUNZI WA MARA SEKONDARI KUREJESHWA MAKWAO, WAZRI KAWAMBWA ATAKIWA KUFANYA UCHUNGUZI



Wednesday, November 27, 2013

SAID HAROUN: Watanzania bana!!!!! Kama Bendera tunafuata upepo...


DR. MKUMBO: UDHAIFU WA MTENDAJI MKUU MSAIDIZI (ZITTO) UNAREKEBIKA KULIKO WA MKUU ALIYEPO (MBOWE)

KATIKA moja ya mambo yaliyojitokeza katika mgogoro wa uongozi wa Chadema, ni tathmini ya nguvu za aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto dhidi ya kinachoitwa udhaifu wa Mwenyekiti wa sasa wa chama hicho, Freeman Mbowe na uongozi wake.

Tathmini hiyo ambayo aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dk Kitila Mkumbo jana ameiita kuwa ni siri iliyowekwa wazi kwa makosa ya kijinga, imeeleza namna kiongozi huyo alivyoandaa mkakati wa kumuondoa Mbowe madarakani kidemokrasia, kupitia nguvu za Zitto
“Nani tumuunge mkono kuchukua nafasi ya Mkuu (Mbowe).Utangulizi huo (udhaifu wa Mbowe) unaoonesha kinagaubaga kwamba tunahitaji mabadiliko na hatua iliyofuata ilikuwa ni kuangalia nani anaweza kuleta mabadiliko tunayohitaji. “Ni vema ikazingatiwa kwamba mtu ambaye tungemuunga mkono lazima awe mwenye uwezo mkubwa kuliko tunayetaka kumtoa (Mbowe).

Awe ana sifa za kiuongozi na zaidi sana awe na uwezo wa kupambana na mkuu aliyeko. “Katika kuchunguza ndani ya taasisi (Chadema), tuliridhika kwamba Mtendaji Mkuu Msaidizi (Naibu Katibu Mkuu, Zitto), ana sifa zote tulizozitaja hapo juu ingawa kila mwanadamu ana udhaifu wake.

“Ni dhahiri pia kwamba udhaifu wa Mtendaji Mkuu Msaidizi unarekebika kuliko wa mkuu aliyepo,” umeeleza mkakati ambao Dk Mkumbo amekiri kuuandaa na kusisitiza hajutii kazi hiyo aliyoiita ni ya matamanio ya mabadiliko ndani ya Chadema.

KAIRUKI ATAKA USHIRIKIANO KUUKABILI UNYANYASAJI

Washiriki mbalimbali wa maendeleo na wadau wa masuala ya jinsia wametakiwa kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia vinafikia tamati.

Rai hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angellah Kairuki wakati akizindua siku 16 za kupinga ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.
Sambamba na uzinduzi huo Kairuki alizindua pia mfumo wa utoaji wa huduma kwa mfumo wa One Stop Center ambao unajumuisha huduma zote muhimu kwa watakaokutana na ukatili wa kijinsia kama vile polisi, afya na ustawi wa  jamii kutolewa sehemu moja.
Alisema licha ya kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikiongezeka kila kukicha, ni asilimia 4 tu ya kesi hizo ndiyo huripotiwa katika vyombo vya sheria hali inayochangia wahusika kuendelea kuwa huru mitaani.
“Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali katika kuhakikisha vitendo hivi vinatokomezwa, lakini wanawake ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo wamekuwa wakinyanyasika hawakimbilii kutafuta msaada wa kisheria” alisema Kairuki.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF), Naomi Kaihura alisema licha ya kuwepo kwa jitihada mbalimbali za kupinga vita vitendo vya ukatili, changamoto kubwa inabaki katika upatikanaji wa fomu za polisi ambazo hutoa kibali kwa muathirika kupata matibabu.
Alisema hali hiyo kwa kiasi kikubwa inachangia waathirika kupoteza maisha na wengine kukata tamaa ya kutoa ripoti kuhusiana na ukatili waliofanyiwa.
“Ukiritimba katika upatikanaji wa PF3 ni changamoto kubwa hali inayosababisha  waathirika kupoteza maisha hata kabla hawajapata matibabu,” alisema.

CHANZO: MWANANCHI

Tuesday, November 26, 2013

JAMII YATAKIWA KUTUMIA NAFASI ZILIZOPO KUPAMBANA NA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE



Na Butije Hamisi- Mwanza

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ernest Mangu Ameitaka jamii na kila mtu kutumia nafasi alonayo kuzuia ukatili wa kijinsia ili kuboresha afya ya jamii.
Ameyasema hayo katika uzinduzi wa siku 16 za kupambana na ukatili dhidi ya wanawake uliofanyika jana katika viwanja vya line polisi Mabatini jijini Mwanza.
Kamanda Mangu amesema kanda ya ziwa inaongoza kwa matukio ya kikatili nchini, hivyo watu wote hawana budi kuamka kupambana na ukatili huo.
“Uwepo wa matukio hayo unaleta haja ya walio katika nafasi kusimama na kuzuia vitendo vya ukatili” alisema kamanda Mangu
Kamanda mangu amesema mkoani mwanza mpaka sasa matukio ya mauaji ya kishirikina yamefikia 40 na watu 44 wakipoteza maisha katika matukio hayo wanawake wakiwa ni 34 na wanaume 10 tu. Huku watuhumiwa 133 wakishikiliwa na jeshi la polisi.
Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa shirika la KIVULINI Bw. Ramadhan Masele  amesema kampeni hiyo ya siku 16 inalenga kuamsha ari kwa watanzania kupambana na ukatili wa kijinsia hususan kwa wanawake na kauli mbiu ya kampeni hiyo ni “Funguka ! Tumia mamlaka yako, zuia ukatili wa kijinsia, kuboresha afya ya jamii.
Bw. Masele amebainisha kuwa kukosekana kwa sheria maalumu inayohusika na ukatili wa kijinsia, mitazamo hasi ya jamii dhidi ya wanawake, ukosefu wa huduma bora za afya na vitisho kwa wahanga wa ukatili ni baadhi ya changamoto zinazo wakabili katika harakati za kupambana na ukatili wa kijinsia.
Pia Diwani wa kata ya Mbugani Bw. Hashim Hassan Kijuu ameitaka jamii kushirikana katika ngazi zote toka familia, mtaa mpaka taifa kupambana dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Shirika la KIVULINI limekuwa likendesha harakati za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto na siku ya November 25 ya kila mwaka ni siku ya kimataifa ya kupambana na ukatili dhidi ya wanawake duniani.

Sunday, November 24, 2013

TAARIFA YA ZITTO KABWE KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHADEMA

TAARIFA YA ZITTO ZUBERI KABWE (MB) KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHAMA CHANGU CHA CHADEMA

1. Utangulizi 

Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 - 22 Novemba 2013, Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. Kwa mujibu wa taarifa ya chama iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana kama mkakati wa uchaguzi 2013. Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha Kamati Kuu . Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa Taifa. Nitazianisha tuhuma hizi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vyama.

Ninatambua kwamba chama changu kinapita katika wakati mgumu sana sasa hivi. Nataka nitamke mapema sana kwamba mimi Zitto Zuberi Kabwe sitokuwa chanzo cha CHADEMA kuvunjika. Hiki ndicho chama kilichonilea na kunifikisha hivi nilivyo. Ningependa chama hiki mtoto wangu atakapokuwa mtu mzima na atakapoamua kujiunga na siasa aingie CHADEMA. Bado nina imani kubwa na chama changu na ninaamini ndicho kinachostahili kuendesha nchi jana, leo na kesho. 

2. Kuhusu tuhuma mbalimbali zinazo elekezwa kwangu

Zipo tuhuma nyingi ambazo zimekuwa zikirudiwarudiwa katika vikao vya chama na nje ya vikao na baadhi ya viongozi wenzangu. Tuhuma hizi zinalenga kuonyesha kwamba mimi ni mbinafsi na kwamba ninapokea rushwa ili kukihujumu chama changu. Nitazianisha tuhuma kwa kifupi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vya chama. 

i) Tuhuma kwamba sikushiriki kumpigia kampeni mgombea wetu wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2010. Ningependa kueleza yafuatayo kuhusu jambo hili:

Saturday, November 23, 2013

BUTIJE: KARIBUNI KATIKA MAHAFALI



ZITO NA DR. KITILA KUKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI KUTOA MSIMAMO WAO JUU YA KUVULIWA NYADHIFA ZAO NDANI YA CHADEMA


DR. KITIMA: MITAZAMO TOFAUTI SIO USALITI NI DEMOKRASIA


UBAKAJI NA ULAWITI HAVIKUBALIKI


Monday, November 4, 2013

DIVISION 5 HAIONGEZI MAABARA, VITABU, WALIMU WALA KUBORESHA MASLAHI NA MAZINGIRA YA WALIMU


Sunday, November 3, 2013

LEMA: UNAFIKI WA ZITTO KABWE NA SUALA LA POSHO

UNAFIKI WA ZITTO KABWE NA SUALA LA POSHO – LEMA

Kama nilivyosema jana kuwa leo kabla ya saa nane mchana nitaweka wazi unafiki wa Zitto katika suala la posho , suala ambalo halihitaji vikao vya Chama kulijadili isipokuwa vyombo vya habari na hususani mitandao ya kijamii kama yeye anavyofanya na kujaribu kupotosha ukweli na kutafuta sifa ambazo kimsingi hana.

CHADEMA wakati inaamua kulijadili suala hili la posho , msingi wake mkuu ulikuwa kama ifuatavyo :

1)
CHADEMA iliona na kutambua ubadhirifu unaofanyika kupitia kivuli cha posho katika Taasisi za Umma na Serikali na sio Bunge pekee , hivyo CHADEMA ikapendekeza mishahara ipandishwe na posho zisizo za lazima ziondolewe ili kuondoa mwanya wa ubadhirifu wa fedha za Umma .Huu ndio uliokuwa msimamo wetu .


Kulikuwa na msingi mkuu ambao ungekuwa na faida kubwa kwa Nchi na Watu wake lakini kabla msimamo huu haujawekwa hadharani na kutafsiriwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni , Zitto Kabwe tayari alishatoka katika vyombo vya habari ni kujipambanua kuwa yeye hataki posho na wala hatachukua posho , na hapa vyombo vya habari vilichukua jambo hili kama hoja yake binafsi na huku mantiki ya hoja kamili ikipotea . ( Mantiki ilikuwa ni kuondoa posho zisizo za msingi kwa Watumishi wote wa Umma na kuboresha masilahi yao kwa maana ya mishahara )

Lengo kubwa la Kambi Rasmi ya Upinzani inayoongozwa na CHADEMA ni kupigania masilahi bora ya Watumishi wa Umma na Sekta binafsi katika Nchi hii . Msingi wa CHADEMA ulikuwa na maana pevu kwani tulijua kama mishahara ikiongezwa itampa fursa Mtumishi kuwa na Maisha bora leo na hata baadaye kwa mafao bora baada ya utumishi wake kazini . Lakini ingekuwa rahisi pia kwa Mtumishi kuwa na uwezo mkubwa wa kutafuta mikopo kwa ajili ya maendeleo kwani Mabenki yanatoa mikopo kupitia mishahara ya Watumishi . Ikumbukwe kwamba , mtumishi mwenye mshahara mzuri anakuwa na fursa ya kupata mkopo mkubwa ambao utatatua matatizo yake mengi . Kwa hiyo msingi wa kutaka posho zisizo na msingi ziondolewe ilikuwa ni mkakati wa CHADEMA kuboresha masilahi ya Umma kupitia mishahara .

Niliposema Mh Zitto ni mnafiki kuhusu suala hili , nilikuwa na maana ifuatavyo :

ZITTO: MBUNGE ANAELILIA POSHO HASTAHILI...AKATAFUTE KAZI NYINGINE



JUA/MWEZI/UMEME



Friday, November 1, 2013

UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU KIDATO CHA 4 NA 6


MGOMO WA MADAKTARI WALIOKO MAFUNZONI WANUKIA: BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA AFYA, Mh.Dr. Hussein Mwinyi

BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA AFYA,
Mh.Dr. Hussein Mwinyi


Kwa heshima kubwa, Sisi madaktari na wafamasia tuliopo mafunzoni (Internship) katika hospitali za mikoani tofauti na Muhimbili tunapenda kukutaarifu Mh.Waziri wa Afya,kwamba kumekuwepo na matatizo katika malipo ya posho tunazolipwa kila mwezi.Matatizo hayo ni kuwepo kwa tofauti ya malipo kati ya wale wanaofanya mafunzo ya vitendo katika Hospitali ya Muhimbili na wale wanaofanyia hospitali zilizopo mikoani na tofauti na Muhimbili.

Wakati wenzetu wa Muhimbili wanalipwa 100%,yaani 1,225,000/= kwa madaktari na 994,000/= kwa wafamasia,sisi wa mikoani na nje ya Muhimbili tunalipwa 80% yaani 980,000/= kwa madaktari na 795,200/= kwa wafamasia.
Tumejaribu kufuatilia tofauti hiyo kuanzia mwezi julai lakini hatujapata jibu linaloeleweka kwani ilidaiwa kwamba kulikuwa na makosa ya kiutendaji yalifanyika lakini kwa bahati mbaya mpaka leo tunakuandikia barua hii bado tatizo hilo linaendelea.

Kwa barua hii,tunaomba majibu yaliyokamilika na sahihi kutoka kwako Waziri wa Afya na kwamba tunajiandaa kugoma endapo ufumbuzi wa tatizo hilo hautafanyika kwa wakati kwa sababu hatua ya kutofautisha malipo siyo tu ya unyanyasaji lakini pia ni ya kibaguzi na inavunja katiba yetu ya nchi.
Ni matumaini yetu kwamba madai haya yatafanyiwa kazi ipasavyo na hatimaye kupewa stahiki zetu kama ilivyo kwa wenzetu wa Muhimbili.


NAKALA· Chama cha madakatari Tanzania· Baraza la Famasi· Gazeti la Mwananchi· IPP media· Freemedia Group · Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

Dar es salaam-Kinshasa Railway lazima ijengwe

Sasa Tanzania imejifunza vitu vingi.
Siasa ni mfumo wa kiuchumi ambso utawainua wananchi husika.
Siasa ya Tanzania kwa nchi za nje kwa miska mingi imekuwa ya ukombozi, ukombozi wa mwafrika toka tawala za kikandamizi za kikoloni.

Hivi karibuni Tanzania imejikuta katika sakata la kuitetea Kongo na wananchi wake walioko mashariki mwa Kongo.

Wananchi hawa kwa miaka mingi wamekuwa katika mlolongo wa matatizo ya kukosa amani na ustawi wa jamii.

Umoja wa mataifa umejaribu kwa miongo mingi tu kuleta amani bila mafanikio.
Lakini ni katika jaribio la mwisho hili la kutumia nguvu kwa kuwashirikisha majirani wa Kongo wenye nia ya dhati kuisaidia, sasa tunaona amani yaweza kurejea mashariki ya Kongo.

Ni wazi kuwaTanzania haina chake ndani ya Afrika Mashariki kutokana na hatua za wazi za kutengwa na majirani zetu wa kaskazini.

Lakini akufungiaye njia anakuonyesha mlango mzuri zaidi , hata ni kama wa kuufanyia kazi zaidi.

Ni vema sasa watanzania tukaweka mguu ndani ya Kongo, mguu wa kibiashara, mguu ambao hautaondolewa na tsifa lolote..

Ni muhimu sasa wananchi wa Kongo na Tanzania tukawa wamoja na kuendeleza spirit ya Goma, spirit ya ushirikiano kibiashara sasa.

Kilichobaki ni kuendeleza reli ya kati hadi Kigoma. Na kuanzisha rail ferries hadi mashariki mwa Kongo na kushinikiza wenzetu wa Kongo ku ifungua nchi yao kwa kujenga reli hadi Kinshasa.

Utajiri mkubwa wa Kongo na Tanzania utakuwa kichocheo kikubwa sana katika kujenga reli hii.

I have a dream!!!

CHANZO:  http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/