Wednesday, August 28, 2013

SIMBA, AZAM ZAIBUKA KIDEDEA, YANGA YABANWA MBAVU NA COASTAL UNION

Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva (kushoto) akipiga shuti huku beki wa Coastal, Juma Nyoso, akijaribu kumdhibiti, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom  kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, imeendelea leo katika viwanja tofauti na mabingwa watetezi, Yanga SC wamelazimishwa sare ya 1-1 na Coastal Union, huku Simba SC wakiishinda JKT Oljoro 1-0 mjini Arusha wakati Azam FC wakishinda bao 2-0 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora.

Mbeya; Wenyeji Mbeya City wameshinda 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Mabao ya wenyeji yalifungwa na Paul Nonga dakika ya saba na Steven Mazanda dakika ya 90, wakati bao la Ruvu lilifungwa na Shaaban Suzan dakika ya 24. 

Tanga; Bao pekee la Fully Maganga dakika ya 62, lilitosha kuipa Mgambo JKT ushindi wa 1-0 dhidi ya Ashanti United kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Chamazi; Kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Dar es Salaam, JKT Ruvu iliendeleza wimbi la ushindi baada ya kuilaza Prisons 3-0. Mabao ya JKT yalifungwa na Machaku Salum dakika ya 44, Emmanuel Swita dakika ya 69 na Hussein Bunu dakika ya 87


Tuesday, August 20, 2013

MAHAKAMA YA MISRI YAAMURU MUBARAK AACHIWE HURU


 

Mahakama ya Misri imeamuru kuachiliwa huru aliyekuwa raisi wa nchi hiyo aliyepinduliwa madarakani kwa maandamano ya wananchi Hosni Mubarak.
Mahakama hiyo imesema kuwa hakupatwa na hatia katika kesi iliyokuwa imebakia ya ubadhilifu. Kwa mujibu wa wakili wake na duru za mahakama za Misri, korti imeamuru Mubarak aachiliwe huru katika kesi ambayo yeye na watoto wake wawili Alaa na Gamal walikuwa wakituhumiwa kufanya ubadhilifu wa fedha za umma.

Taarifa hiyo inasema kwamba, Mubarak anaweza kuachiliwa huru wiki hii, lakini watoto wake wawili wataendelea kushikiliwa. Huko nyuma pia iliamriwa kwamba  Mubarak aachiliwe huru katika kesi nyingine mbili ambapo alishitakiwa kuhusika katika mauaji ya waandamaji wakati wa harakati za maandamano ya mwaka 2011 ambayo yalimuaondoa madarakani na pia kujilimbikizia mali kinyume cha sheria.